Mlinzi wa klabu ya Everton Yerry Mina atakuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki kumi kutokana na mejeruhi aliyoyapata, kocha wa timu hiyo Frank Lampard athibitisha hilo.
Mchezaji huyo wenye miaka 27 anaecheza nafasi ya ulinzi wa kati, alilazimika kutoka kipindi cha kwanza kwenye mchezo wa jumanne wa ligi kuu ya Uingereza, dhidi ya Newcastle United ambao walipoteza.
Frank Lampard wakati anatoa taarifa hizo alisema “nilikuwa natambua ni kwa kiasi gani tatizo lake ni kubwa, na sasa ile hofu yetu imethibitishwa sasa, kwa bahati mbaya majeruhi ya Yerry Mina yatumuweka nje kwa wiki nane mpaka kumi, ni majeruhi makubwa sana kwenye kikosi chetu kwa sasa.
“wiki iliyopita ndio nilitambua Yerry Mina ni kiongozi mwenye umuhimu mkubwa kwetu, ananafasi kubwa sana hapa, ni mtu asiye na matatizo na tutamkumbuka.”
Everton wameshinda mchezo mmoja tu kati ya michezo 15 ya ligi waliyocheza na Jumamosi wanakutana na Leeds United kwenye dimba la Goodison Park.