Thu, 21 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mlinzi wa pembeni Yao Kouassi ana hatihati kuukosa mchezo wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika wakati timu yake ya Yanga SC itakapowavaa mabingwa wa Afrika Kusini, Mamelodi Sandown.
Akitoa taarifa ya majeruhi waliopo kwenye kikosi, Afisa wa Yanga Ali Kamwe amesema, nyota huyo tegemeo kikosini mpaka sasa ana asilimia hamsini kuwepo na hamsini kutokuwepo.
"Yao yeye ni hamsini kwa hamsini, alipata majeraha ya nyama za paja bado anaendelea na matibabu na kwa mujibu wa daktari wetu ni hamsini kwa hamsini kuwepo kwenye mchezo wetu dhidi ya Mamelodi," alisema Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live