Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezo wa Yanga SC Azam FC uliopelekwa mbele kwa siku moja kupisha mchezo wa Mashindano ya African Football League, sasa utachezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Jijini Dar es Salaam, Oktoba 23.
Awali mchezo huo ulipangwa kuchezwa Oktoba 22 katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Taarifa za kuaminika ilizozipata Manara Tv zimesema kuwa pambano hilo la Ligi Kuu Bara litapigiwa katika uwanja huo uliokuwa umefungwa kupisha marekebisho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: