Wed, 8 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara Timu ya Yanga imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC kwa kufikisha alama 24 baada ya michezo 9.
hiyo ni baada ya kuichapa Coastal Union bao 1-0 katika mchezo mgumu uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Bao pekee la ushindi la Yanga katika mchezo wa leo limefungwa na Clement Mzize alieingia kutokea benchi akichukua nafasi ya Kennedy Musonda.
Bado mambo yanazidi kuwa magumu kwa Coastal Union ambao katika michezo yao 9 wamshinda mchezo mmoja pekee.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: