Fri, 21 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Yanga imeulizia huduma ya mshambuliaji wa klabu ya TP Mazembe ambaye yupo kwa mkopo katika klabu ya Al-Itihad, Jean Othos Baleke.
Wakala wake, Augustino Ikandilo amethibitisha kuwa klabu ya Yanga wameulizia huduma ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka (23).
Baleke ligi kuu msimu huu 23|24:
Mechi 10 ⚽ 8 - Simba SC
Mechi 10 ⚽ 7 - Al-Itihad.
Yanga SC wanampango wa kuachana na washambuliaji wake, Joseph Guede ambaye anamaliza mkataba mwezi huu na Kennedy Musonda ambaye anatakiwa na klabu ya Tout Puissant Mazembe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live