Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga yashusha viingilio mechi ya Marumo Gallants

Yangaaaaa Gsh Yanga yashusha viingilio mechi ya Marumo Gallants

Fri, 5 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Afisa Habari ya Yanga SC Ally Kamwe kupitia mkutano na waandishi wa habari hii leo ameeleza kuwa Viingilio vya Mshabiki kushuhudia mchezo wa Nusu Fainali Kombe la Shirikisho CAF Barani Afrika dhidi ya Marumo Gallants FC kutokea Afrika Kusini vimeshushwa kwa namna ya kipekee kabisa ili mashabiki na wadau wa klabu hio waweze shuhudia mechi hio Wiki ijayo siku ya Jumatano.

Amesema kwamba za Tiketi VIP A zitapatikana kwa Tzs. 30,000/=, VIP B 20,000/= na VIP C ni Tzs. 10,000/=, Tiketi ya Mwisho ni ya Mzunguko ambayo ni Tzs. 3,000.

Ameongeza kuwa Tiketi za mzunguko zitalipiwa kwa Tzs, 3,000 kwa siku kabla ya (kutokea leo hadi jumanne) kufikia siku rasmi ya mchezo lakini ikifika siku husika tiketi zitanunuliwa kwa Tzs. 5,000 kwa lengo la kuwapa nafasi mashabiki kama zawadi ya kipekee kutoka Uongozi wa Klabu hio pia maeneo ya kukatia tiketi yaongezwa ili kuwa na utaratibu wa kukata tiketi mapema kalba ya siku ya mchezo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: