Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga yapaa viwango vya CAF, yaiacha mbali Simba

Simba Yanga WA0007 Yanga yapaa viwango vya CAF, yaiacha mbali Simba

Thu, 29 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirikisho la Soka Africa CAF limetoa orodha ya viwango vya ubora wa vilabu Africa ambapo Klabu ya Yanga imepanda kutoka (18) hadi nafasi ya (11) kwa msimu wa 2024/25.

Kiwango cha klabu kinapanda kutokana na mafanikio yake katika mashindano 2 vilabu vya CAF; Ligi ya Mabingwa wa CAF na Kombe la Shirikisho la CAF.

Timu inayopokea pointi zaidi katika msimu uliopita itachukuliwa kuwa timu iliyo kwenye nafasi ya juu. [13]

Vilabu vilivyoorodheshwa kwa Ligi ya Mabingwa ya CAF 2024-25 na Kombe la Shirikisho la CAF 2024-25 itatokana na matokeo kutoka kwa kila shindano la vilabu la CAF kuanzia 2019-20 hadi msimu wa 2023-24.

01. Al-Ahly - Alama 72

02. Wydad Athletic - Alama 55

03. Mamelodi Sundowns - Alama 49

04. Esperance de Tunis - Alama 46

05. Petro de Luanda - Alama 39

06. Raja Casablanca - Alama 35

07. TP Mazembe - Alama 33

08. Zamalek - Alama 33

09. RS Berkane - Alama 32

10. CR Belouizdad - Alama 32

11. Young Africans - Alama 31

12. USM Alger - Alama 31

13. ASEC Mimosas - Alama 30

14. Simba SC - Alama 29

15. Pyramids - Alama 29

16. JS Kabylie - Alama 22.

CR Belouizdad imeporomoka kutoka (7) hadi (10) baada ya kushindwa kufuzu hatua ya Robo Fainali ya CAFCL huku timu zilizofuzu robo fainali zikisogea juu ikiwemo Yanga, TP Mazembe, ASEC na nyingine.

Simba SC imeshuka licha ya kwamba inayo nafasi ya kurejea top (10) endapo itafanikiwa kuingia robo fainali atafikisha points (39) katika nafasi ya (6).

Msimu wa (21/22) Klabu ya Yanga ilikuwa na points (0.5) CAF, baada ya misimu (2) wamekusanya points (31). Yanga wanazidi kupanda kwa kasi.

Simba akiingia robo fainali points zitakuwa hivi; Yanga SC atakuwa amekusanya alama 31 kwa miaka miwili wakati Simba atakuwa amekusanya alama 39 kwa miaka mitano.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live