Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga yanpa 'Thank you' Augustine Okrah

Augustine Okrah Augustine Okrah

Thu, 4 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo mshambuliaji raia wa Ghana, Augustine Okrah, hatakuwa sehemu ya kikosi cha Young Africans msimu ujao 2024-2025.

Nyota huyo ambaye amewahi kuichezea Simba SC msimu mmoja, alitua Young Africans Januari 2024 akitokea Bechem United ya Ghana na kuitumikia timu kwa kipindi cha miezi sita.

Okrah licha ya kucheza Young Africans kwa muda mfupi wa miezi sita, lakini mchango wake umeonekana katika mafanikio ya timu.

Kiungo huyo anaondoka Young Africans akiwa ameshinda ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC na Kombe la CRDB Bank Federation msimu wa 2023-2024 na kuwa sehemu ya kikosi kilichocheza robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari ya Yanga imeelza; "Young Africans SC tunamtakia kila la kheri Okrah katika safari yake ya soka."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live