Wed, 16 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Yanga Usiku wa Jana walishuka uwanjani kuwavaa Biashara United katika mchezo wa hatua ya 16 Bora Kombe la Azam Sports Federation.
Kabla ya Mchezo huo, wachezaji wote wa Yanga walivaa jezi zenye Jina la nyota wao wa zamani Ally Mtoni "Sonso" aliefariki Dunia Februari 11 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Baada ya tukio hilo wachezaji waligawa jezi hizo kwa Mashabiki, kama ilivyo kawaida ya klabu hiyo.
Tazama hapa chini kuona namna Yanga walivyoomboleza tukio hilo.
Pumzika Kwa Amani Ally Mtoni Sonso
— Young Africans SC (@yangasc1935) February 15, 2022
Wananchi Tutakukumbuka Daima????#DaimaMbeleNyumaMwiko pic.twitter.com/EFg21VCEh6
Chanzo: www.tanzaniaweb.live