Wed, 3 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mazungumzo kati ya Klabu ya Yanga na mshambuliaji Kennedy Musonda yamefikia hatua kubwa sana ili mchezaji aweze kuondolewa katika klabu hiyo kuelekea msimu ujao.
Makubaliano ya mwisho yatatolewa hivi karibuni baada ya kikao cha mwisho kitakachokaa wikendi hii ili mchezaji huyo aweze kupishana uhamisho wa wachezaji wapya ambao watakuja kuboresha eneo la ushambuliaji.
Ikiwa makubaliano yatakamilika basi Kennedy Musonda ataondolewa kikosi ikiwa makubaliano hayajakamilika basi ataendelea kuhudumu, ripoti ya Miguel Gamondi ni kuhitaji maboresho ya eneo la ushambuliaji kwa mchezaji wa kigeni.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live