Tue, 5 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha timu ya Yanga kimmeondoka asubuhi ya leo kuelekea nchini Ghana kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama.
Yanga watatupa karata yao ya tatu dhidi Medeama siku ya Ijumaa saa 4:00 usiku katika kampeni ya kusaka kwenda robo fainali.
Kundi hilo linaongozwa na Al Ahly wenye alama 4, CR Belouizdad alama 3, Medeama alama 3 huku Yanga ikishika mkia kwa alama moja pekee
Chanzo: www.tanzaniaweb.live