Fri, 27 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kama kawa, kama dawa Yanga SC wameendeleza ubabe mbele ya Singida FG kwa kuwashushia kipigo cha goli 2-0.
Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani wa kutosha hususan kipindi cha pili, ilipigwa leo Oktoba 27, 2023 katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
Magoli hayo ya ushindi yaliwekwa kimiani na Max Nzengeli dakika ya 30 na dalika ya 39 ya mchezo.
Yanga wameendelea kujikita kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC kwa kufikisha alama 18 wakiwa wamecheza michezo saba. Hii si mara ya kwanza Yanga kuifunga Singida kwani tangu waingie Ligi Kuu, hawajawahi kuifunga.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live