Bingwa mtetezi wa wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), Young Africans 'Yanga'wameshusha kipigo kikubwa kwa Kurugenzi FC kwenye mchezo wa raundi ya pili ya michuano ya kombe hilo.
Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye Dimba la Mkapa jioni ya lwoz Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa bao 8-0 sawa na ushindi ambao walipata wapinzani wao Simba dhidi ya Eagle Fc jana.
Yanga walipumzisha mastaa wao karibu wote wa kikosi cha kwanza wengi na kuwapa nafasi wachezaji ambao wamekuwa hawapati nafasi za kuanza katika kikosi cha mwalimu Nasreddine Nabi.
Straika kinda na mzawa ndani ya Yanga, Clement Mzize amefanikiwa kuondoka na mpira baada ya kufunga bao 4 peke yake katika mchezo huo.
Wafungaji; ⚽⚽⚽⚽ Clement Mzize dakika ya 1' 8' 42' na 45+4'
⚽ Jefta John (goli la kujifunga) dakika ya 5'
⚽ David Bryson dakika ya 77'
⚽⚽ Yusuf Athumani dakika ya 78' na 85'
Matokeo ys mechi za leo
FT Yanga SC 8-0 Kurugenzi FC
FT Tz Prisons 7-1Misitu FC
FT Siginda Big Stars 2-0 Lipuli FC
FT KMC 6-1 Tunduru Korosho FC
FT Kigoma Kwanza 0-1 Buhaya FC
FT Namungo FC 2-2 Kitayosce FC (Penalty 3-1)
FT Polisi TZ 3-0 Nyika FC
FT Mtibwa Sugar 2-0 TRA FC
VIPIGO VIKUBWA ASFC RAUNDI YA PILI
1. Azam Fc 9-0 Malimao
2. Ihefu Sc 9-0 Mtama Boys
3. Simba Sc 8-0 Eagle Fc
4. Yanga 8-0 Kurugenzi Fc
6. Tz Prisons 7-1 Misitu Fc
7. KMC 6-1 Tunduru Korosho
8. Mbeya city 5-1 Stand Fc.