Klabu ya Yanga imejibu taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa kiungo mshambuliaji Clatous Chama hana furaha ndani ya kikosi hicho kutokana na kocha Miguel Gamondi kutomwanzisha kwenye kikosi cha kwanza tangu asajiliwe kutoka Simba.
Taarifa hizo zimekuwa zikidai kuwa, kwenye mkataba wake na Yanga, Mwamba wa Lusaka anatakiwa kuanza kikosi cha kwanza iwapo atakuwa fit na hana majeraha wala tatizo lolote.
Msemaji wa Klabu ya yanga, Ally Kamwe amesema; "Hakuna kipengele kinachotaka Chama aanze, na sio Chama tu , mchezaji yoyote wa yanga hakuna kipengele kinachotaka aanze Kikosi cha kwanza. Hizo ni propaganda watu wameanzisha kwa sababu wanatafuta faraja," amesema Ally Kamwe.