Ofisa habari na mawasiliano wa Klabu ya Yanga Ali Kamwe akiyazungumzia mashindano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika amedai Klabu ya Yanga SC ni wenyeji kabisa wa mashindano hayo, hivyo watakuwa wenyeji na kuwakaribisha Klabu ya Azam FC ambao nao wamefuzu kushiriki katika mashindano hayo.
Msimu uliopita Yanga iliishia katika hatua ya Robo Fainali na Mamelod Sundowns kwa mikwaju ya penalti baada ya kutoka suluhu ya 0-0 katika uwanja wa Benjamin Mkapa lakini pia nchini Afrika Kusini.
Kauli ya Kamwe hii na mara ya Yanga kushiriki kwa mafanikio mashindano ya CAF kwa misimu miwili mfululizo, msimu wa 2022-23 wakimaliza hatua ya Fainali kwenye Kombe la shirikisho na msimu wa 2023-24 kuishia hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.