Wed, 1 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wananchi wametinga hatua ya nusu fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB (CRDB Federation Cup) kufuatia ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Tabora United katika dimba la Azam Complex, Chamazi.
Pacome Zouzoua aliyekuwa nje kwa takribani mwezi na nusu, amejerea na kuweka pasi moja ya goli, ubora ni ule ule amerejea na makali yake.
FT: Yanga SC 3-0 Tabora United
⚽ Stephanie Azizi Ki 35'
⚽ Kennedy Musonda 66'
⚽ Joseph Guede 83'.
Yanga sasa itakutana na Ihefu kwenye hatua ya nusu fainali. Ihefu imefuzu kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kuwaondoa Mashujaa FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live