Tarifa za ndani zinasema kuwa Mabosi wa Yanga sasa wako kwenye hatua za mwisho kumboreshea mkataba kiungo fundi Maxi Nzengeli, ikiwa ni pamoja na kumpa gari la kisasa atakalokuwa anatanua nalo mjini, jambo ambalo halikuwepo kwenye mkataba wa awali aliokubaliana nao.
Hesabu hizo hazitakuwa kwa Nzengeli pekee, pia beki wao wa kulia Kouassi Yao ambaye amekuwa kwenye kiwango kikubwa, wawili hao wakithibitisha ubora wao ndani ya muda mfupi kwenye kikosi hicho ambacho msimu huu kitacheza Ligi ya Mabingwa Afrika.
Maxi ametua Yanga akitokea AS Maniema ya Kongo, huku Yao akitokea ASEC Mimosas ya Ivory Coast.