Wananchi Yanga SC, wameamua kupunguza bei ya jezi zao kama ofa ya Sikukuu ya Eid lakini pia kuongeza hamasa kwenye mchezo wao wa Robo Fainali Kombe la Shirikisho Afrika.
Aakizungumza na wanahabari leo Aprili 19, 2023, Afisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe, amesema jezi hizo za kimataifa zenye mdhamini tofauti na zile za Ligi Kuu, zilikuwa zikiuzwa shilingi elfu hamsini lakini sasa zitauzwa elfu arobaini.
"Hii ni ofa kwa mashabiki wetu kwani tucheza mchezo wetu wa kwanza wa Robo Fainali Kombe la Shirikisho Jumapili Aprili 23, 2023 siku ambayo itakuwa ndani ya shamrashamra za Sikukuu ya Idd," alisema Ally.