Klabu ya Yanga itakipiga dhidi ya klabu ya CR Belouizdad Ijumaa hii 24 November 2023 katika uwanja wa Stade 5 Juillet 1962.
Kumbuka, Yanga SC walicheza fainali ya CAFCL katika uwanja huu dhidi ya klabu ya USM Alger ambayo ni miongoni mwa vilabu vyenye mashabiki wengi zaidi Nchini Algeria,
UWANJA: Uwanja ulijaa (Full-house), waliingia watazamaji takribani elfu sitini na sita (66).
Yanga waliibuka na ushindi wa bao 1 , lakini wakashindwa kutwaa kombe kutokana na kanuni ya goli la ugenini.
Ijumaa hii wanarejea tena katika uwanja huo. Mchezo utachezwa saa 4:00 Usiku kwa saa za Afrika mashariki na saa 2:00 Usiku kwa saa za Nchini Algeria.
Kwa maana hiyo Yanga hawana ugeni na Uwanja huo na huenda wakaendeleza kile walichokifanya mara ya mwisho walipofika nchini humo.