Wed, 15 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Young Africans ipo kwenye harakati za kuifukuzia saini ya kungo Najim Mussa kiungo wa Tabora United
Hii ni baada ya Azam FC na Simba SC kubisha hodi kwa kiungo huyo fundi, na sasa ni rasmi Yanga nao wametuma ofa ya kutaka kuhitaji huduma yake kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi.
Mipango ya Eng. Hersi Said ni kutaka kumaliza dili mapema kabla ya michezo ya ligi kuu ambapo Malengo ya Yanga ni kusajili wazawa wenye ubora wa hali ya juu.
Najim kwa sasa yupo chini ya usimamizi wa Wakala anayewasimamia wa Bakari Mwamnyeto, Zawadi Mauya na Kibu Denis.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live