Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga walifanikiwa hapa dhidi ya Ihefu ngumu

Pacome 183305558 Pacome Zouzoua.

Mon, 20 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kuna wakati unahitaji wachezaji waweze kukusimamia kwa ustadi wa hali ya juu kushinda mipambano yao dhidi ya mpinzani aliyeimara sana , ndicho walichofanya wachezaji wa Yanga kuweza kumsimamia Miguel Gamondi kwa dakika 120 na kushinda mechi, kwa nini?

1: Wachezaji wote walikuwa karibu karibu sana iliwasaidia sana kuweka presha kwenye mpira wakipoteza (counter pressing), na hii kusaidia kudumisha mashambulizi (sustain attack)

2: Waliamua kuufanya uwanja kuwa mpanza ili kumtanua mpinzani wao zaidi (Ihefu), kwasababu alicheza nyuma na kupiga (lowblock)

3: Walikuwa na idadi ndogo ya pasi ndefu ndefu bali walitumia sana one touch football ili kumove safu ya Ulinzi ya Ihefu , repeatedly walifanikiwa sana

Ihefu wamepoteza mechi lakini wamefanya vitu vingi kwa usahihi , na kwa wakati sahihi : waliacha distance ndogo sana kwenye mstari yote mitatu na hii iliwapa faida kuzuia na kushambulia kwasababu walikuwa karibu karibu sana

YANGA wanabadilika sana , ukiweza kushinda mipambano yao kwa kiasi katika basi watabadilisha kutafuna spaces zilizo wazi pembeni (jinsi goli lilivyopatikana).

Kumbuka;

1: Yule Tanimu ni beki mzuri sana, wala hapaniki na wala hahofii kujaribu tena

2: Aucho kuna vipass fulani hivi alikuwa anapiga, mithiri ya Iniesta

3: Ondogo ni bonge la beki, energy nzuri sana

4: KI Aziz kwenye mita 25 ya mwisho ya uwanja ni hatari sana , anafunga tu

5: Zouzoua ni game changer wa maana kabisa

6: Energy na strength ya Attohoula Yao

FT: Ihefu FC 0-1 Young Africans.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live