Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga wakubali kuwauza Aziz Ki, Diarra na Bacca

Aziz Diarra 0002 Yanga wakubali kuwauza Aziz Ki, Diarra na Bacca

Tue, 9 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hiki sasa ni kiburi! Uongozi wa Klabu ya Yanga umeeleza kuwa wapo tayari kumuuza Max Nzengeli pamoja na wachezaji wengine wowote wanaofanya vizuri endapo itatokea timu inawahitaji.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ali Kamwe ametoa kauli hiyo alipokuwa Afrika Kusini walipokwenda kuwavaa Mamelodi Sundowns katika mchezo wa pili ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa awali uliopigwa Benjamini Mkapa Stadium.

“Sisi hatuna hofu ya wachezaji wanaofanya vizuri kuondoka, tulimuuza Fiston Mayele akiwa mfungaji bora hivyo sisi hatuna shida. Wakitokea watu wanawahitaji wataweka mpunga tutaleta wachezaji wengine na maisha yataendelea kama kawaida,” alisema Kamwe.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live