Fri, 24 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka Bongo, Edgar Kibwana amesema, endapo Yanga SC watapoteza mchezo wa leo, wasisingizie kuchelewa kwa vifaa vya mazoezi walivyovisahau kwenye ndege.
“Popote unapoanza unaweza kufanya vizuri kwa namna ambavyo umejiandaa ndani na nje ya uwanja, kwa Yanga ndio wanaanza na inawezekana mjumbe amezungumza kwa nia njema kwamba vifaa vimechelewa lakini watu wasichukulie kama sababu kama Yanga itafungwa kesho (leo)”
Kibwana amechambua hivyo baada ya kutoka kwa taarifa ya kwamba vifaa vya mazoezi vimechelewa na kufanya kikosi kishindwe kuanza mazoezi kwa wakati kama ilivyopangwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live