Fri, 4 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Yanga SC, imekanusha taarifa za kwamba wanatarajia kucheza na AS Vita kutoka nchini Kongo.
Akizungumza na Wasafi FM, Afisa Habari na Mawasiliano, Ally Kamwe, amesema taarifa hizo ziliibuka mitandaoni na zimeishia mitandaoni.
"Hizo taarifa zimeanzia mitandaoni na zimeishia hukohuko mitandaoni. Sisi hatuna ratiba na mechi nyingine yoyote public zaidi ya maandalizi yetu dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Jamii," alisema Ally Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live