Mon, 25 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Yanga SC wametangaza mechi ya dhidi ya Mamelodi itakuwa ni Muda Day wakimaanisha kumpa kiuongo wao Mudathir Yahya kuwa ndio mechi yake.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ali Kamwe amesema Mudathir Yahya ndiye wamempa mchezo huo hivyo wachezaji wote watatakiwa kuendana na kasi ya Mudathir.
"Ukimtazama Muda tu utajua Yanga wanakwendaje, simu zile anazopiga Mudathir basi ziite simu, watu pia waitane kuja Benjamini Mkapa siku hiyo kushuhudia kile tunachokwenda kukifanya," alisema Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live