Tue, 6 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu NBC, Timu ya Yanga kimeanza safari kuelekea Ruangwa Mkoani Lindi kujiandaa na mchezo dhidi ya Namungo FC.
Yanga waliofika jana Mkoani Mtwara, waliweka kambi na leo msafara umeondoka kuelekea Ruangwa.
Mpaka sasa Yanga inaongoza msimamo wa Ligi wakiwa na alama 35 baada ya kucheza michezo 14 sawa sawa na Azam wakiwa na tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Tazama msafara wa kikosi cha Yanga,
Kikosi kimeondoka Mtwara kuelekea Ruangwa tayari kwa mchezo wa kesho dhidi ya Namungo FC. #TimuYaWananchi #DaimaMbeleNyumaMwiko pic.twitter.com/1bkl9Bggsf
— Young Africans SC (@yangasc1935) December 6, 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live