Klabu ya Yanga Ikiwa imebakiwa alama 10 pekee ili iweze kuutetea ubingwa wa Ligi kuu kandanda Tanzania Bara kwa mara nyingine tena kati ya alama 18 ambazo klabu hiyo imebakiza,
Kwa hesabu za kawaida Yanga inahitaji kushinda michezo mitatu (3) walau na sare moja (1), kati ya michezo sita (6) ambayo klabu hiyo imebakiza hadi hivi sasa.
Msimu uliopita Yanga walitangaza Ubingwa mbele ya Dodoma Jiji katika mchezo uliopigwa kwenye Dimba la Chamazi huku Yanga wakiibuka na ushindi wa bao 4-2 huku Mudathir Yahya akitupia bao 2.
Matokeo hayo yatategemea michezo ijao ya wapinzani wao wanaowafuata.
Azam Fc
Mechi 24
Alama 54
Simba Sc
Mechi 22
Alama 47
Michezo ijayo ya Yanga
vs Mashujaa - A
vs Kagera - H
vs Mtibwa Sugar -A
vs Dodoma Jiji -A
vs Tabora United -H
vs TZ Prison -H.