Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga kufanya maamuzi magumu

Aziz KI X Skudu Yanga kufanya maamuzi magumu

Thu, 2 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kwa mujibu wa almachiuskanyasi Klabu ya Young Sports Club ilikwishaanza Mazungumzo ya kuwaongezea Kandarasi baadhi inatamatika na wanahitajika klabuni Wachezaji hao ambao Mikataba yao.

Farid Mussa - Ni kweli mkataba wake unatamatika mwishoni mwa msimu huu ila mpaka muda huu hakuna mazungimumzo yoyote yaliyoanza.

Zawadi Mauya - Kweli mkataba wake unatamatika mwishoni mwa msimu huu ila imefahamika kuwa Klabu ya Yanga haina Mpango wa kuendelea kuwa nae.

Denis Nkane - Mwisho wa Msimu huu atakuwa Mchezaji huru na imefahamika kuwa klab yake ya Yanga haina Mpango nae tena.

Nickson Kibabage - Yes ameshaongeza mkataba mpya wa Miaka 3 baada ya ule wa Mkopo kutamatika.

Clement Mzize - Mkataba wake na Young Africans ulikuwa unaelekea ukingoni ila tayari ameshaongeza kandarasi ya miaka 2.

Makudubela Skudu - Ameshataarifiwa kuwa klab ya Yanga hakina Mpango nae kuelekea Msimu ujao.

Kibwana Shomari - Kweli Mkataba wake na Yanga unaelekea ukingoni ila Mazungumzo ya Mkataba mpya yameanza na klab yake licha ya kuwa tayari ana ofa 3 mkononi mwake.

Bakar Mwamnyeto - Mazungumzo ya mkataba mpya yameanza na muelekeo wake mzuri, tayari alikuwa na ofa za vilabu viwili vikimuhitaji.

Joyce Lomalisa - Ni kweli Mkataba wake unaelekea tamati na hakuna mazungumzo yoyote ya kuongeza kandarasi Mpya mpaka muda huu.

Metacha Mnata - Kandarasi yake na Klabu ya Yanga inaelekea mwishoni kabisa ila bado hakuna mazungumzo ya mkataba mpya.

Pacome Zouzoua - Ni kweli amesaliwa na mkataba wa mwaka mmoja ila klabu yake imepanga kumuongezea miaka miwili zaidi.

Aziz Ki - Mkataba wake ukiwa ukingoni taarifa za ndani ya uongozi wa Yanga zinadai alishaongeza kandarasi na waajiri wake ambao ni Yanga.

Kuna uwezekano kuna wachezaji Wazawa wasiopungua 3 wataachwa baada ya mikataba yao kuisha na wapo wakigeni pia wasiopungua 4 ili kupisha maingizo mapya.

Imefahamika kuwa Klabu ya Yanga itasajili wachezaji wasiopungua 4 wakigeni, washambuliaji wawli, kiungo mmoja na Mlinzi wa kushoto 1 hao ndio wanawanchi kuelekea dirisha kubwa la usajili.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live