Wed, 6 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Young Africans inaendelea na mazoezi yake katika mji wa Kumasi kujiandaa na mchezo wake wa Ligi ya mabingwa Barani Afrika dhidi ya Medeama utakaopigwa Ijumaa hii.
Kwa mujibu wa ripoti ya Daktari wa klabu hiyo amesema klabu hiyo itamkosa Joyce Lomalisa pekee aliyeumiakatika mchezo dhidi ya Al Ahly.
Joyce Lomalisa atakaa nje ya uwanja kwa takribani wiki moja ili kurejea mazoezini tena.
Yanga inakamata nafasi ya mwisho katika msimamo wa kundi lake ikiwa na alama moja na ushindi dhidi ya Medeama utawafanya kuibua matumaini ya kusonga Robo Fainali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live