Wed, 1 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Soka Barani Afrika limeitaja Klabu ya Yanga kuwania Tuzo ya Klabu Bora ya Mwaka 2023 kwa Wanaume Barani Afrika.
Yanga SC itachuana na Klabu za CR Belouizdad, USM Alger, Asec Mimosas, Al Ahly, Raja CA, Wydad AC, Mamelodi Sundowns, Marumo Gallants na ES Tunis katika kinyang'anyiro hicho.
Tuzo hizi zitatolewa Desemba 11, 2023 Jijini Marrakesh, Morocco
Tazama hapa chini Timu zinazowania Tuzo hiyo;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live