Kipa namba mbili wa kikosi cha Yanga, Aboutwalib Mshery, amesema alichojifunza ndani ya Young Africans ni kuwa bingwa na kuendelea kupambania ndoto.
Kauli ya Mshery imekuja ikiwa hii ni mara yake ya tatu mfululizo kubeba ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC tangu alipoanza kuvaa jezi ya Young Africans Desemba 2021.
“Msimu huu ulikuwa mzuri sana, tumepambana kutoka mwanzo mpaka hapa leo tumechukua ubingwa kwa sababu mwisho wa msimu unatakiwa kuwa na kitu na kitu chenyewe ndio hiki kwa hiyo ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu.
“Ndani ya Yanga nilichojifunza ni kuwa bingwa, nashukuru sana kwa hilo,” alisema Mshery.