Mon, 8 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa masuala ya soka kutoka TV3, Alex Ngereza amesema kuwa iwapo Yanga iliyocheza na na APR ya Rwanda ingecheza na Simba basi Yanga wangefungwa bao nyingi.
Yanga ilifungwa bao 3-1, na APR na kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi katika hatua ya robo fainali.
"Yanga wana bahati, wangekutana na Simba kwa jinsi ambavyo wamecheza leo (jana) wangepigwa sio chini hata ya goli tano.
"Yanga wapunguze maneno wanaongea sana wakati hawawezi kufanya vitendo baada ya kupangwa na APR waliongea sana wakasahau kujiandaa mwisho wa siku wamefungwa goli tatu," amesema Alex Ngereza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live