Tue, 19 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka nchini, Farhan Kihamu amesema Yanga SC kufika fainali ya Shirikisho Afrika si mafanikio.
Amesema hata Simba SC nao hawajafanikiwa kwenye soko la Kimataifa bali wamepiga hatua.
“Yanga kufika fainali (CAFCC 2022/23) ni kupiga hatua hawajafanikiwa, timu zetu kwenye mashindano ya kimataifa hakuna aliyefanikiwa wamepiga hatua tu.
“Simba leo hii kuingia makundi sio stori, kucheza robo sio stori wenyewe wanahitaji nusu fainali, kuna siku watahitaji fainali na wakibeba ubingwa watakuwa wamefanikiwa,” alisema Farhan.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live