Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga Yaifunika Simba kwa Rekodi ya Dk 2,520

Yanga Picha Yanga Yaifunika Simba kwa Rekodi ya Dk 2,520

Sat, 22 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

KLABU ya Yanga imekuwa ikitengeneza rekodi na kuzitikisa timu pinzani ikiwemo Simba, Azam na nyingine, kwani kwa sasa ndiyo timu pekee ambayo haijaonja kipigo kwenye ligi msimu huu.

Yanga wanatamba na rekodi ya kucheza michezo mingi zaidi msimu huu kuliko timu yoyote tangu msimu huu kuanza, wamecheza jumla ya mechi 31, wakishinda 24, sare nne na kufungwa mechi tatu. Wakifunga mabao 53, wao wakiruhusu 14 tu.

Huku rekodi wanayowatesea Simba ni ile ya kucheza mechi 28 sawa na dakika 2,520 bila kupoteza. Tena kubwa zaidi wakiwa wao pekee hawajafungwa kwenye ligi msimu huu wakati Simba wenyewe wamefungwa juzi tu.

Yanga wamecheza mechi 12 za ligi kuu, wakishinda mechi tisa, sare kwenye mechi mbili, wakifunga mabao 20, wakiruhusu manne. Wamecheza mechi 12 za kirafiki wakishinda zote, mechi tatu za Mapinduzi Cup walishinda moja, sare kwenye mechi mbili, na moja ikiwa ya nusu fainali wakitolewa kwa matuta na Azam FC.

Wamecheza mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika, wakifungwa zote na Rivers United ya Nigeria, mchezo mmoja wa Ngao ya Jamii dhidi ya Ihefu wakishinda 4-0.

Mechi za kirafiki 12, wameshinda 11 na kufungwa mechi moja tu, dhidi ya Zanaco ya Zambia mabao 2-1 kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi huku wakiwa hawajatoka sare kwenye mechi hata moja ya kirafiki.

Hivyo Yanga walifungwa na Rivers mara mbili na kufungwa na Zanaco mara moja ndani ya dakika 90. Sare za Yanga ni ile ya 1-1 na Namungo, pamoja na suluhu dhidi ya Simba na kule Mapinduzi Cup sare ya 2-2 na KMKM.

Kwa upande wa Simba wao wamecheza jumla ya mechi 20, mechi 11 za ligi kuu, mechi nne za kimataifa na michezo mitano ya kirafiki. Simba Ligi ya Mabingwa walicheza mechi mbili.

Walikipiga dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana mechi mbili kwenye hatua za kwanza za mashindano hayo, walishinda ugenini 2-0 na kufungwa nyumbani 3-1.

Kisha wakacheza na Red Arrows Kombe la Shirikisho. Wakafungwa ugenini 2-1 mechi ya pili, wakati mechi ya kwanza walishinda 3-0 nyumbani. Kwa ujumla kwenye mechi zote msimu huu Simba wamefunga mabao 28, wakifungwa mabao 16.

Simba wamefungwa mechi nyingi zaidi msimu huu kuliko Yanga, walifungwa na TP Mazembe 1-0, wakapigwa na Yanga kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii 1-0. Wakatandikwa na Jwaneng Galaxy 3-1. Wakafungwa pia na Red Arrows 2-1.

Rekodi yao ya kucheza bila kupoteza ikiwa ni ya dakika 1,350 sawa na michezo 15, michezo 10 ya ligi kuu, michezo minne ya Kombe la Mapinduzi na mechi moja ya FA.

Walitoka sare ya 2-2 na Far Rabat, kisha 1-1 na Olympique De Khouribga zote za Morocco. Wakaenda sare ya 2-2 na Cambiaso, Sare na Coastal Union, sare na Biashara United kisha kwenda suluhu na Yanga yote kweli ligi kuu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live