Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga, Simba kuanzia raundi ya pili CAF 2024/25

Simba X Yanga CAF Yanga, Simba kuanzia raundi ya pili CAF 2024/25

Tue, 4 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msimu wa mashindano ya CAF Interclub 2024/25 utaanza kwa raundi ya awali kati ya tarehe 16 Agosti hadi 18 Agosti, 2024 huku hatua za makundi zikipangwa kufanyika kati ya mwezi Oktoba hadi mwezi Desemba mwaka 2024.

Klabu ya Yanga itaanza kampeni zake za Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye raundi ya pili michuano hiyo na wataanzia ugenini huku Simba Sc ikianzia raundi ya pili ya kombe la Shirikisho Afrika nayo itaanzia ugenini.

Azam Fc itaanzia raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika huku Coastal Union wakianzia raundi ya kwanza ya kombe la Shirikisho Afrika.

Azam Fc na Coastal Union wataanzia nyumbani kwenye michuano hiyo ambayo inaanza kurindima kuanzia Agosti 16 mpaka 18.

Tanzania ni miongoni mwa Nchi 12 pekee za Afrika zitakazoingiza timu nne kwenye mashindano ya CAF. Nchi nyingine ni Algeria, Angola, Ivory Coast, Misri, Libya, Morocco, Nigeria, DR Congo, Afrika Kusini, Sudan na Tunisia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: