Mon, 30 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Haya sio matokeo ya mechi ya Simba SC na Yanga SC hapana, bali ni mahesabu ya tofauti ya idadi ya ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya miamba hao wa soka nchini.
Kimahesabu ni Yanga anaongoza 7-0 mbele ya Simba, kwani kutokana na rekodi ya Ubingwa huo, Yanga wamebeba ubingwa mara 29 na Simba mara 22, ukikokotoa hapo Yanga anakuwa anaongoza kwa makombe 7 mbele ya Simba.
Jumapili ijayo ni dabi ya Kariakoo kati ya Simba na Yanga, mchezo wa Ligi utakaopigwa katika Dimba la Mkapa.
Swali ni je, msimu huu nani atabeba ubingwa?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: