Yanga Princess wameamua kuiboresha timu yao baada ya Rais wa Yanga SC, Eng. Hersi Said kuamua kuweka nguvu pia kwenye timu ya Wanawake.
Wamemsajili mchezaji bora (MVP) wa ligi kuu ya Nigeria ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Nigeria Toluwalashe Adeshola.
Mpaka sasa Yanga Princess wametangaza majina ya wachezaji (4) wakigeni kama ifuatavyo:
Rita Akarekor ➜ Golikipa timu ya Taifa Nigeria.
Uzoamaka Igwe Confidence ➜ Beki wa kati timu ya Taifa ya Nigeria. CAF Bronze medalist
Toluwashe Adeshola ➜ Kiungo timu ya Taifa Nigeria. ➜ (MVP) ligi kuu ya Nigeria.
Danai Bhobho ➜ Kiungo timu ya Taifa Zimbabwe.
Usajili unaendelea.
Yanga Princess wanautumia uwanja wa (KMC) katika maandaliziyao.