Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga, Nabi jino kwa jino Ligi ya Mabingwa

Nabi X Yanga Yanga, Nabi jino kwa jino Ligi ya Mabingwa

Sun, 27 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakati Yanga ikifuzu kwa jeuri hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikitupa nje ASAS ya Djibouti kocha wao wa zamani Nasreddine Nabi naye amepita njia hiyohiyo kibabe.

Yanga imewatupa nje ASAS kwa ushindi wa jumla wa mabao 7-1 wakitangulia kushinda mechi ya kwenda kwa mabao 2-0 kisha jana kumaliza kibabe mchezo wa pili kwa mabao 5-1.

Nabi ambaye kwasasa anaifundisha FAR Rabat ya ambao ni mabingwa wa Morocco naye akitangulia kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 ugenini nchini Togo dhidi ya ASKO Kara ya huko kisha kushinda nyumbani kwa mabao 7-0 Jana usiku.

Yanga kwenye ushindi huo imetoa mwamba mmoja Maxi Nzengeli aliyeweka kambani mabao mawili kwenye mchezo wa pili dakika wakati Nabi ametoa mastaa watatu waliofunga mabao kama hayo.

Kwenye ushindi wa Jana washambuliaji Lamine Diakite aliyefunga mara moja kwenye kila mchezo,Ahmed Hammoudan beki Anour Tarkhatt wote walifunga mara mbili timu yao ikifuzu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: