Shoo ya kipindi cha pili, ilikuwa ya jasho si Yanga wala Mtibwa Sugar, zilikuwa zinapambana kupata bao.
Kuna uwezo wa wachezaji binafsi na bato zilizobamba, wachezaji kupambania timu zao kupata pointi tatu, mchezo huo ulipigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, leo Jumamosi ya Februari 20, 2021 ambapo Yanga imeijipatia pointi tatu baada ya kushinda bao 1-0 lililofungwa na CarlosĀ Fernandez 'Carlinhos'.
Mwanaspoti Online linakuchambulia bato za wachezaji waliotoana jasho katika harakati zake za kuwania pointi tatu.
Kisinda vs Baba Ubaya
Beki namba tatu wa Mtibwa Sugar, Issa Rashid alipata kazi kubwa ya kudhibiti mbio za Miongoni Tuisila Kisinda aliyekuwa na kasi ya kwenda langoni kwao.