Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga, Mbeya City washushiwa rungu TFF

Morrison Yanga Byeee Yanga, Mbeya City washushiwa rungu TFF

Thu, 29 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Mbeya City imetozwa faini ya Tsh laki tano (500,000) kwa kosa la watoto waokota mipira kuchelewa kwa makusudi kurejesha mipira kiwanjani kwenye mchezo wa sare ya 3-3 dhidi ya Yanga uwanja wa Sokoine.

Sambamba na hilo Mbeya City imetozwa faini Tsh milioni moja (1,000,000) kwa kosa la mashabiki wake kuwarushia chupa wachezaji wa Yanga wakati wakishangilia moja ya mabao waliyofunga.

Aidha klabu ya Yanga imetozwa faini ya Tsh milioni moja (1,000,000) kwa kosa la mashabiki wake kuwarushia chupa walinzi wa uwanjani kwenye mechi hiyo ambayo Yanga ililazimika kutoka nyuma 3-0 na kusawazisha magoli yote kunusuru alama moja kwenye sare ya 3-3.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: