Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga, Azam kupigwa usiku

Usiku Pic Data Yanga, Azam kupigwa usiku

Wed, 21 Apr 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya mabadiliko ya muda wa mchezo wa Ligi Kuu baina ya Yanga na Azam, Aprili 25 kwa kusogeza mbele muda wa mechi kuanza kwa saa 2:15 kutoka muda uliokuwa umepangwa mwanzoni wa saa 1:00 usiku.

Taarifa iliyotolewa na TPLB leo imeeleza kuwa mabadiliko hayo ya muda wa kuanza kwa mechi yamefanyika kutokana na Uwanja wa Benjamin Mkapa ambao utatumika kwa mechi hiyo kuwa na matumizi mengine.

"Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Na. 251 kati ya Yanga na Azam utachezwa saa 2:15 usiku Aprili 25, 2021 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa badala ya saa 1:00 usiku kama ilivyotangazwa hapo awali.

Sababu ya mabadiliko hayo ni uwanja huo kuwa na matumizi mengine mchana," ilifafanua taarifa hiyo ya TPLB.

Timu hizo zitakutana huku Azam FC ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa bao 1-0 katika mechi ya kwanza ambayo walikuwa nyumbani Uwanja wa Azam Complex iliyochezwa Novemba 25, bao pekee la ushindi likipachikwa na Deus Kaseke.

Siku hiyo ya Aprili 25 ambayo Yanga na Azam FC zitaumana, pia kutakuwa na mechi nyingine mbili siku hiyo ambapo Ihefu wataialika Coastal Union na Prisons watacheza na Ruvu Shooting

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz