Fri, 12 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Azam FC, Yahya Zayd, amefanyiwa upasuaji wa goti kutibu tatizo la 'Meniskasi' ya ndani na pembeni.
Upasuaji huo uliofanikiwa, ulifanyika huko Afrika Kusini kwenye hospitali ya Life Vincent Pallotti, jijini Cape Town.
Kwa upasuaji huo, Zayd atakaa nje ya uwanja hadi majuma sita, kabla ya kurudi uwanjani.
Tunamuombea apone haraka na kurudi kwenye majukumu yake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live