Wed, 16 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
DAKTARI wa viungo wa Yanga, Mtunisia, Youssef Ammar, amesema kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Yacouba Songne, amepata nafuu na atarejea uwanjani baada ya takribani siku 45.
Yacouba yupo nje ya uwanja tangu Novemba mwaka jana alipoumia goti ambapo tayari amepatiwa matibabu nchini Tunisia.
Ammar alisema Yacouba ameanza program ya mazoezi ya kukimbia mbio fupi na ndefu kwa ajili ya kujiweka sawa, ikiwa ni baada ya kumaliza program ya gym.
Aliongeza kuwa nyota huyo atakuwa fiti na kamili kuanza kuipambania timu hiyo, baada ya mwezi mmoja na nusu ambao ni sawa na siku 45.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live