Wed, 10 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
NYOTA wa Yanga SC raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne amepelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wao wa ligi dhidi ya Ruvushooting.
Songne anaesumbuliwa na jeraha la goti huenda akawa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi mitatu kutokana na ukubwa wa jeraha hilo.
Sogne anaelekea kwenye miezi sita ya mwisho ya mkataba wake ndani ya Yanga lakini kocha Nabi bado anamuhitaji kikosini na Yanga wapo kwenye mazungumzo ya kumpa mkataba mpya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live