Katika kujiweka sawa na mechi ya ligi kuu,timu ya wananchi Yanga SC leo Jumatano saa 1:00 usiku wataingia dimba la Azam Complex Chamazi kucheza mechi ya kirafiki na KMKM.
KMKM inakuwa ni timu ya pili kutoka Zanzibar kuelekea Tanzania Bara kwaajili ya kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi cha mabingwa wa kihistoria Yanga SC.
Yanga ilicheza mchezo wa kirafiki na kikosi cha Mlandege Sep 16, 2020 na mchezo huo timu ya Mlandege ilikubali kufungwa magoli 2 kwa mzunguko na kikosi cha Yanga SC.
Katika mchezo huo timu ya Yanga ilipata ushindi kwa wa mchezaji wake Wazir Junior dakika ya 40 na Tunombe Mukoko nae alilipachika mnamo dakika ya 59.