Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Xavi majaribuni wikendi hii

Xavi MC Mobile Kocha mpya wa Barca, Xavi Hernandez

Thu, 18 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mashabiki wa sehemu mbalimbali duniani kwa sasa wanasubiri kumuona Xavi akiwa kwenye benchi la Barcelona na kubeba mzigo uliowashinda wenzia kwenye viunga vya Camp Nou.

Baada ya kufanya vizuri nchini Qatar na style ya "tiktak" ambayo iliasisiwa na Johan Cryuf na kutumiwa vizuri kabisa na kocha wa kihispania Pep Gurdiola sasa mashabiki wanahamu ya kuona Xavi akiirudisha tena kwenye viunga vya Camp Nou.

Barcelona wikiendi hii wanawakaribisha klabu ya Espanyol kwenye dimba la Camp Nou huku baadhi ya wachezaji nao wakirejea kutoka kwenye michezo ya kimataifa na wale majeruhi Pedri na Dembélé wakitarajiwa kurudi kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Benfica.

Xavi tokea achukue mikoba ya kuinoa klabu hiyo amefanya mabadiliko makubwa huku akitumbua majipu ambayo alihisi ni kikwazo kwa mafanikio ya Barcelona.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live