Meneja wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez ameweka wazi kuwa kiungo Sergio Busquets ambaye anahusishwa na kuondoka klabuni hapo Januari ataendelea kusalia klabuni hapo mpaka mwisho wa mkataba wake.
“Busquets ataendelea kuwa nasi hadi mwisho wa mkataba wake mwezi Juni. Kisha tutaona, itakuwa ni uamuzi wake Mambo yakienda vizuri tutajaribu kumshawishi aendelee kusalia”.
“Nadhani dirisha hili la usajili kwetu litakuwa kimya. Nina furaha sana na kikosi cha sasa.” Amesema Xavi
Kiungo Sergio Busquets anatajwa kutaka kutimkia nchini Marekani na siku chache zilizopita alitangaza kustaafu Timu ya Taifa ya Hispania.