Wed, 29 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wapinzani wa Simba kwenye Hatua ya Makundi ya Klabu Bingwa, Wydad Casablanca, jana Novemba 28, 2023 wamechezea kipigo kizito cha 3-1 kutoka kwa FAR Rabat.
Hiyo ni mechi ya Ligi nchini kwao Morocco, imemalizika na FAR Rabat kuzidi kujisimika kileleni wakiwa na alama zao 20 wakiwa wamecheza mechi 10 huku Wydad wakiwa nafasi ya 7 na alama zao 13.
Kwenye Klabu Bingwa, Wydad ametoka kupigwa tena wikiendi iliyopita na Jwaneng Galaxy 1-0. Kwenye kundi lao Simba SC wapo na Wydad, Jwaneng Galaxy na ASEC Mimosas.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live