Fri, 27 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wydad Casablanca imetinga hatua ya nusu fainali ya African Football League kufuatia ushindi wa jumla wa 4-0 dhidi ya Miamba ya Nigeria, Enyimba FC katika dimba la Mohamed wa 5, Casablanca.
Magoli ya Wydad katika mchezo huo yamefungwa na Ayoub El Amloud 4'Jamal Harkass 38', Attiyat Allah 43'.
Wydad ilishinda 1-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza huko Nigeria kabla ya kushusha kipondo cha 3-0 nyumbani na kuifuata Esperance ya Tunisia kwenye nusu fainali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live