Wakati Simba SC ikilazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya Asec Mimosas, Vigogo wa Morocco, Wydad wakiwa nyumbani Mohamed V, Casablanca wamekubali kichapo cah 1-0 dhidi ya Wababe wa Simba SC, Jwaneng Galaxy ya Botswana katika mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Goli la pekee na la ushindi la timu ya Jwaneng Galaxy katika mchezo huo limefungwa na Sesinyi dakika ya 33'.
Mara baada ya mchezo huo vyombo vya habari kutoka nchini Morocco vimeishutumu timu ya Jwaneng Galaxy kutumia ushirikina katika mchezo huo
MSIMAMO KUNDI B 1. Jwaneng (3) 2. Asec Mimosas (1) 3. Simba SC (1) 4. Wydad AC. (0)